Chepngetich alenga taji la mbio za kilomita 10 Romania – Taifa Leo
Written by Black Hot Fire Network on September 23, 2024
Mwanariadha wa Kenya Janet Chepngetich. PICHA | MAKTABA
WAWANAWAKE saba kutoka Kenya akiwemo bingwa wa Michezo ya Afrika wa mbio za mita 10,000, Janet Chepngetich watashiriki mbio za kilomita 10 za tRUNsylvania zitakazofanyika mjini Brasov nchini Romania mnamo Septemba 22.
Chepngetich ni mmoja wa watimkaji wanaopigiwa upatu kutwaa taji.
Atawania tuzo ya Sh644,300 akikabiliwa na upinzani kutoka kwa Wakenya wenzake Loice Chemnung, Christine Njoki, Nelvin Jepkemboi, Judy Kemboi, Grace Loibach Nawowuna na bingwa wa Afrika, Gladys Kwamboka.
Pia, kuna Waethiopia Yeshaneh Anley, Lemlem Hailu, Lemlem Alemu, Godu Tekle . . .