Kwani Kenya ni jukwaa la ‘vipindi’ hatari? – Taifa Leo
Written by Black Hot Fire Network on April 11, 2025
Punda 'anayecheka'. Picha|Hisani
NINA rafiki ambaye hunicheka nikishangilia mchezo wa kandanda, na nikimuuliza sababu ya kunicheka ananicheka zaidi.
Tabia yake hiyo hainiudhi, hunisababishia kicheko zaidi, sote wawili tukajipata tukiangua kweli-kweli!
Aliwahi kunieleza eti alipoteza imani na mchezo huo alipogundua kuwa ni ‘kipindi’ kinachoandaliwa na wasimamizi kwa ajili ya kuendeleza biashara.
Anaamini hata matokeo ya mechi zote hupangwa tangu mwanzo kwa mapenzi ya wafadhili, yaani zile kampuni kubwa-kubwa zilizo na biashara ambazo hutokea kwenye runinga mechi zikiendelea.
Yeye ni shabiki sugu wa raga, sikwambii na . . .