‘Macuzo’ watamtatiza Ruto – Taifa Leo
Written by Black Hot Fire Network on June 10, 2025
Aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua. Picha|Maktaba
NILIKUWA kati ya watu waliodhania kuwa aliyekuwa naibu Rais Rigathi Gachagua angezama kabisa kisiasa baada ya kufukuzwa kazi mwaka uliopita.
Bunge la taifa lilidhania kuwa ana tabia ovyo zisizoafiki taasisi ya Urais.
Bunge la seneti angalau likampa alama chache japo ratili ya tuhuma zilizokuwa zikimkabili ikawa nzito.
Mtoto wa Maumau jinsi anavyopenda kujiita akaambiwa kanyaga kubwa kubwa kama wanavyosema vijana wa leo.
Akaondoka kwa masikitiko, uso wake ukaonyesha mtu aliyelemewa na mzigo mzito wa siasa.
Wachache waliosalia naye . . .