Mashabiki waomba walipiwe nauli kwenda na Harambee Stars mechi ya Malawi – Taifa Leo
Written by Black Hot Fire Network on May 29, 2024
Mashabiki waomba walipiwe nauli kwenda na Harambee Stars mechi ya Malawi
MASHABIKI wa soka nchini kupitia chama chao (KEFOFA) wamelilia serikali, Shirikisho la Soka Kenya (FKF) na wahisani wakitaka ufadhili kuisapoti Harambee Stars katika mechi za kufuzu Kombe la Dunia 2026 nchini Malawi mwezi ujao.
Kenya itavaana na Burundi mnamo Juni 7 na kisha ichapane na mabingwa wa Afrika Cote d’Ivoire mnamo Juni 11 katika mechi za Kundi E uga wa Mbingu wa Mutharika.