Mihic akiri presha inamlea, Gor ikiendea Mara Sugar KPL leo – Taifa Leo

Written by on April 27, 2025

Kocha mpya wa Gor Mahia Sinisa Mihic akiringisha jezi yake mnamo Februari 3, 2025. Picha|Hisani

KOCHA wa Gor Mahia Sinisa Mihic Jumamosi  alikiri kuwa presha inaendelea kumlemea katika juhudi za  klabu ya kutetea taji lake la  Ligi Kuu (KPL).

Mihic, 48 amekiri kuwa wakiendelea kudondosha alama, basi watajipata pabaya na kupoteza taji hilo ambalo Gor imelichukua mara 22.

Mihic atarejea kwenye benchi ya kiufundi ya Gor Jumapili baada ya kukosa sare ya 1-1 dhidi ya Sofapaka na kupigwa 1-0 na limbukeni FC Talanta mnamo Alhamisi uga huo huo . . .



Current track

Title

Artist