Miji ya Afrika ingali nyuma katika kupambana na maradhi sugu – Taifa Leo
Written by Black Hot Fire Network on March 28, 2025
ZAIDI ya watu 4.2 bilioni wanaishi mijini kote duniani kwa sasa huku idadi hiyo ikitarajiwa kuongezeka hadi takriban theluthi tatu ya watu wote kufikia mwaka 2050.
Miji inapoendelea kustawi kumeibuka hatari ya ongezeko la maradhi sugu yasiyoambukiza (non-communicable diseases kwa Kimombo) katika miaka ya hivi karibuni.
“Ongezeko la idadi ya watu, ujenzi wa majumba na barabara pamoja na ongezeko la magari barabarani ni baadhi ya masuala ambayo yamechangia kupanda maradufu kwa maradhi haya,” atanguliza Mkurugenzi wa Idara ya Afya ya Kijamii katika Shirika la Afya Duniani (WHO) , Bw Etienne Krug.
