Mourinho naye pia ajumuishwa katika wanaoweza kuwa kocha mkuu wa Brazil – Taifa Leo
Written by Black Hot Fire Network on April 8, 2025
Kocha Jose Mourinho. PICHA|HISANI
JOSE Mourinho anaaminika kuwa katika orodha ya makocha wa timu ya taifa ya Brazil ambaye inaangalia kujaza nafasi ya kocha mkuu baada ya Dorival Junior kutimuliwa mnamo Machi 28, 2025.
Kocha huyo Mreno, ambaye kwa sasa anatia makali Fenerbahce, yuko katika orodha inayojumuisha pia Mwitaliano Carlo Ancelotti (Real Madrid), Mhispania Pep Guardiola (Manchester City), Wareno Jorge Jesus (Al Hilal, Saudi Arabia) na Abel Ferreira (Palmeiras, Brazil) na Mbrazil-Mwitaliano Renato Gaucho (Fluminense).
Gaucho alijiunga na Fluminense Aprili 3, 2025 kama kocha wake kwa mara ya sita . . .