Onyo kali la AK ikichagua Wakenya 444 kupimwa dawa za kusisimua kabla ya Riadha za Dunia 2025 – Taifa Leo
Written by Black Hot Fire Network on April 3, 2025
Wanariadha wakifanya mazoezi. PICHA|HISANI
SHIRIKISHO la Riadha nchini Kenya (AK) limechagua wanariadha 444 wanaoweza kuwakilisha taifa kwenye Riadha za Dunia mjini Tokyo, Japan mnamo Septemba 13-21, 2025.
Katika taarifa kwa vyombo vya habari hapo Jumatano, Aprili 2, 2025, shirikisho hilo lilieleza kwa kina nani ataruhusiwa kupeperusha bendera ya Kenya kwenye mashindano hayo ya haiba.
AK imesema kuwa mamia hao ya wanariadha watapimwa dawa za kusisimua misuli ili kuhakikisha wako sawa kwa mashindano kwa kutimiza masharti.
“Kifungu cha 15.5.1-3 cha sheria za Shirikisho la Riadha . . .