Tanzania hata wajitanue vifua vipi, wakubali jina la nchi yao limechafuka – Taifa Leo
Written by Black Hot Fire Network on June 3, 2025
Bendera ya Tanzania ikipepea kwenye jengo. Picha|Francis Nderitu
AJABU ya shingo kukataa kulala kitandani! Usiwaamini Watanzania wanapokwambia kuwa hawajali wala kubali kwamba nchi yao imechafuka jina kwa kukiuka haki za kibinadamu.
Wala usiwaamini wakitanua vifua na kudai hawaihitaji jamii ya kimataifa, eti mwonekano wao katika ngazi ya kimataifa si muhimu.
Taifa hilo linaihitaji jamii ya kimataifa kuliko jamii ya kimataifa inavyolihitaji.
Tumeshuhudia wiki nzima ya unoko na matusi ya kila aina kati ya Wakenya na Watanzania kutokana na kisa ambapo wanaharakati wa Kenya na Uganda waliteswa na kutupwa . . .