Tusker yashindwa kuchupa kileleni, ikikabwa sare tasa na Leopards KPL – Taifa Leo
Written by Black Hot Fire Network on May 3, 2025
Mvamizi wa Bandari Alvin Ngoto (aliyevalia shati nyeupe) aruka kuwahi mpira wa juu wakati wa mechi dhidi ya Bidco United ugani Kenyatta, Machakos mnamo Jumamosi. PICHA|BANDARI
TUSKER Jumamosi iliponza nafasi ya kuchupa hadi kileleni mwa msimamo wa jedwali la Ligi Kuu (KPL) baada ya kuagana sare tasa dhidi ya AFC Leopards katika uwanja wa Kenyatta, Kaunti ya Machakos.
Mwanadimba wa Tusker Ian Simiyu alifunga bao dakika ya 87 lakini likafutwa baada ya msaidizi wa refa kuinua bendera kwamba alikuwa ameotea.
Tukio hilo liliwavunja mno moyo mashabiki wa mabingwa hao mara . . .