Vidutu kwenye sehemu za siri vinavyowahangaisha wanaume – Taifa Leo
Written by Black Hot Fire Network on May 2, 2025
Mwanamume akitatizwa na maambukizi katika sehemu za siri. Picha|Maktaba
TAKRIBANI asilimia moja ya wanaume waliopo kwenye mahusiano ya kingono huathiriwa na vipele kwenye sehemu zao za siri baada ya kuathiriwa na ugonjwa unaofahamika kama genital warts.
Vipele hivi visivyo na maumivu huenea kwa kasi hasa kwa wanaume vijana wanaoshiriki ngono. Isitoshe, sababu ya unyanyapaa wa ugonjwa huu, wanaume wengi huwa na wasiwasi mwingi wanapotambuliwa kuugua vipele hivi.
Dkt Muigai Mararo, mtaalamu wa afya ya njia ya mkojo, anaeleza jarida hili kuwa wanaume walio na umri wa miaka 18 . . .