Yote unayopaswa kufahamu kuhusu gonjwa hili – Taifa Leo
Written by Black Hot Fire Network on September 23, 2024
Maambukizi ya Mpox PICHA | MAKTABA
ULIMWENGU umemakinika zaidi kuhusu aina mpya ya virusi vya homa ya nyani (Monkey pox – Mpox) ambavyo vimezidi kusambaa Afrika na kupenya kwa mara ya kwanza Uropa baada ya kuripotiwa nchini Sweden.
Wataalam wametaja aina mpya ya virusi vya mpox kama iliyo hatari zaidi huku Shirika la Afya Duniani (WHO) kwa mara ya pili katika kipindi cha miaka miwili, likitangaza mlipuko unaoendelea kuwa dharura ya afya ya umma duniani.
Kufikia sasa mwaka huu, visa 2,863 vimethibitishwa huku vifo 517 vikirekodiwa huku ikikikadiriwa kuna jumla ya visa . . .