Ajabu bunge la kaunti ya Laikipia kuharibiwa ilhali mswada tata ulikuwa Bunge la Taifa – Taifa Leo
Written by Black Hot Fire Network on June 30, 2024
Afisi za Bunge la Kaunti ya Laikipia zilizoharibiwa Jumanne. Picha|Josiah Mugo
SPIKA wa Bunge la Kaunti ya Laikipia anaendelea kukadiria hasara baada ya vijana waliojiita Gen Z kuvamia, kupora na kuharibu mali ya mamilioni ya pesa katika majengo ya afisi hizo.
Huku maandamano na makabiliano yalipokuwa yanafanyika katika Majengo ya Bunge la Taifa Jumanne Nairobi, makabiliano sawa na hayo yalikuwa yanafanyika Laikipia na kusababisha uharibifu mkubwa na ghasia licha ya kuwa kaunti hazikuwa zinahusika na sheria hiyo tata.
Spika Lantano Nabaala alisema vijana wenye hasira waliojitambulisha kama Gen Z walivamia . . .