Gachagua aomba Uhuru waungane – Taifa Leo
Written by Black Hot Fire Network on May 23, 2024
Gachagua aomba Uhuru waungane
LUCAS BARASA Na MARGARET KIMATHI
NAIBU Rais Rigathi Gachagua kwa mara nyingine tena amemuomba Rais mstaafu Uhuru Kenyatta kuungana naye katika juhudi za kuunganisha eneo na Mlima Kenya.
Haya yanajiri huku Bw Gachagua akishambuliwa vikali na viongozi chipukizi kutoka eneo hilo.
Mnamo Jumanne, Bw Gachagua alimsihi Bw Kenyatta kujiunga naye kuleta umoja katika eneo hilo lililo na wapiga kura wengi.
“Nikiwa kiongozi anayeshikilia wadhifa wa juu kutoka eneo hili, kazi yangu ni kuunganisha viongozi wote wakiwemo wale waliounga Azimio. Tunapaswa kuweka siasa kando . . .