Jeremiah Kioni kuendelea kubeba sufuria kichwani – Taifa Leo
Written by Black Hot Fire Network on March 16, 2024
Jeremiah Kioni kuendelea kubeba sufuria kichwani
NA WANDERI KAMAU
KATIBU Mkuu wa chama cha Jubilee Jeremiah Kioni, amesema hatasitisha kampeni yake ya kuweka sufuria kichwani almaarufu ‘Sufuria Movement’, akisisitiza ataiendeleza hadi pale serikali itapunguza gharama ya maisha nchini.
Kwenye mahojiano na kituo cha redio cha Kameme FM, Bw Kioni alisema kuwa Wakemya wengi bado wanaendelea kuteseka licha ya ahadi za serikali kwamba itapunguza gharama ya maisha.
“Huwa ninabeba sufuria popote ninapoenda. Siko tayari kusimamisha shinikizo hizo dhidi ya serikali hadi pale gharama ya maisha itapungua. Rais William Ruto alitwambia . . .