Maandamano yalivyoanika jinsi ‘ndoa’ baina ya Ruto na Gachagua inavyoyumba – Taifa Leo
Written by Black Hot Fire Network on June 29, 2024
Rais William Ruto na naibu wake Rigathi GAchagua katika hafla ya Maombi ya Kitaifa majuzi. Wawili hao walitoa taarifa kivyao Jumatano kufuatia Majengo ya Bunge kuvamiwa na waandamanaji. Picha|Maktaba
MZOZO kati ya Rais William Ruto na Naibu wake Rigathi Gachagua ulianikwa wazi kufuatia misimamo yao tofauti kuhusu jinsi serikali ilivyoshughulikia maandamano ya kupinga Mswada wa Fedha 2024.
Tofauti na siku za mwanzo za utawala wa Kenya Kwanza ambapo viongozi hao walionekana kushauriana kuhusiana na masuala muhimu ya kitaifa, mnamo Jumatano wawili hao walihutubia taifa kila mmoja kivyake baada ya waandamanaji kuvamia Majengo . . .