Mawaziri watumia kandanda kujipanga? – Taifa Leo
Written by Black Hot Fire Network on January 14, 2024
2027: Mawaziri watumia kandanda kujipanga?
NA WANDERI KAMAU
JE, huenda mawaziri katika serikali ya Rais William Ruto wameanza mikakati ya kujitayarisha kisiasa ielekeapo 2027 kupitia mashindano ya kandanda katika maeneo wanakotoka?
Hili ndilo swali kuu ambalo limeibuka kufuatia hatua ya mawaziri kadhaa kuzindua mashindano hayo.
Baadhi ya mawaziri hao ni Moses Kuria (Utumishi wa Umma), Susan Nakhumicha (Afya), Eliud Owallo (Habari, Mawasiliano na Teknolojia-ICT), Ababu Namwamba (Michezo) na Kipchumba Murkomen (Uchukuzi).