Mechi ya Spurs ilivyoshindia Man-City ligi – Taifa Leo
Written by Black Hot Fire Network on May 20, 2024
Mechi ya Spurs ilivyoshindia Man-City ligi
LIGI Kuu ya Uingereza (EPL) msimu huu imekamilika baada ya kivumbi kikali. Manchester City ndio ni mabingwa na hawawezi kuguswa.
Ushindi wa City dhidi ya Tottenham ambao ni mahasimu wakubwa wa Arsenal, uliweka dhahiri kwamba City, wangetetea ubingwa wao.
Mabao mawili ya Erling Haaland kipindi cha pili yalisuluhisha pambano kali ambalo kipa Stefan Ortega alicheza kama yeye kwenye lango.