Mvutano wa Wetang’ula na Natembeya waanza kutoa usaha – Taifa Leo
Written by Black Hot Fire Network on March 27, 2024
Mvutano wa Wetang’ula na Natembeya waanza kutoa usaha
NA EVANS JAOLA
MAAFISA wanne wa serikali ya Kaunti ya Trans Nzoia mnamo Jumanne walihojiwa katika makao makuu ya Idara ya Kuchunguza Makosa ya Jinai (DCI) katika kaunti hiyo, kutokana na ghasia zilizotokea kwenye hafla moja ya mazishi Ijumaa iliyopita.
Mazishi hayo yalikuwa yamehudhuriwa na Spika wa Bunge la Kitaifa Moses Wetang’ula na Gavana wa Kaunti ya Trans Nzoia George Natembeya.
Wanne hao wanajumuisha msaidizi wa kibinafsi wa Bw Natembeya na Mkurugenzi wa Idara ya Kushinikiza Uzingatiaji wa Sheria . . .