Raila kuokoa jahazi makinda wake wa Azimio wakikwama – Taifa Leo
Written by Black Hot Fire Network on March 23, 2024
Raila kuokoa jahazi makinda wake wa Azimio wakikwama
NA WYCLIFFE NYABERI
KIONGOZI wa Wiper Kalonzo Musyoka, amesema Muungano wa Azimio la Umoja-One Kenya utaendelea kukosoa utawala wa Kenya Kwanza kama kawaida hata ikiwa Raila Odinga anayesifika kwa kuchuna serikali sikio, atapata kiti cha Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika (AUC).
Bw Musyoka alisema upinzani hautabaki kigae na kwamba ikitokea Rais William Ruto anawazidi nguvu na kufinya Wakenya, basi Azimio watatafuta usaidizi wa Bw Odinga hata angalau kwa wiki moja bila kujali ikiwa atakuwa mwenyekiti wa AUC au la.