Arsenal waingia sokoni kutafuta kipa baada ya ligi kuwaponyoka – Taifa Leo
Written by Black Hot Fire Network on May 24, 2024
Arsenal waingia sokoni kutafuta kipa baada ya ligi kuwaponyoka
GEOFFREY ANENE Na MASHIRIKA
ARSENAL FC wanaaminika kuwa sokoni kutafuta kipa wakati huu Mwingereza Aaron Ramsdale anaonekana anaelekea kuondoka uga wa Emirates baada ya kupoteza nafasi yake kama kipa nambari moja.
Soko litafunguliwa Juni 14 hadi Septemba 2, 2024.
Taarifa nchini Uholanzi zinadai kuwa Wanabunduki hao ambao walitumia Mhispania David Raya kwa kipindi kikubwa cha msimu 2023-2024 kwa mkopo kutoka Brentford, sasa wanasemekana kummezea mate Justin Bijlow.
Kipa huyo Mholanzi mwenye umri wa miaka 26 anachezea Feyenoord . . .