Kipchoge mawazo na moyo wake wote ni Olimpiki pekee – Taifa Leo
Written by Black Hot Fire Network on April 18, 2024
Kipchoge mawazo na moyo wake wote ni Olimpiki pekee
MSHIKILIZI wa zamani wa rekodi ya mbio za wanaume za kilomita 42, Eliud Kipchoge, amesimamisha shughuli zake zote kumakinikia kutetea taji lake la Olimpiki kwenye makala ya 33 jijini Paris, Ufaransa mnamo Julai 26 hadi Agosti 11.
Kipchoge, 39, ambaye ametawala marathon katika makala mawili mfululizo, pia alieleza kuwa mwelekeo hasi na ukabila vinaumiza taifa, lakini akasema kuwa wanamichezo wanaweza kurekebisha hali.