Mwanamume akejeliwa kwa kuruhusu mkewe kupanga uzazi – Taifa Leo
Written by Black Hot Fire Network on March 28, 2024
Mwanamume akejeliwa kwa kuruhusu mkewe kupanga uzazi
NA FRIDAH OKACHI
WAVUMISHAJI wa afya ya jamii katika wadi za Heilu na Manyatta zilizoko mjini Moyale, Kaunti ya Marsabit, wanazidi kupata pingamizi katika juhudi zao za kueneza ujumbe wa umuhimu wa upangaji uzazi.
Hali hii inasababishwa na misimamo ya wanajamii kutokana na mafundisho ya kidini, utamaduni wao na pia wanasiasa kuwahimiza kuzaana ili maeneo yao yawe na wingi wa watu.