Ni mapambano ya piga nyofoa kombe la Europa Liverpool wakisaka muujiza – Taifa Leo
Written by Black Hot Fire Network on April 18, 2024
Ni mapambano ya piga nyofoa kombe la Europa Liverpool wakisaka muujiza
PAMBANO kubwa linasubiriwa ugani Olympic Stadium jijini hapa Alhamisi usiku AS Roma itakapoalika AC Milan katika mkondo wa pili wa robo-fainali ya UEFA Europa League.
Chini ya aliyekuwa ya jagina wa klabu hiyo, Daniele De Rossi aliyeteuliwa mwezi Januari kuwa kocha mkuu, AS Roma imeimarika kwa kiasi kikubwa huku ikiandikisha matokeo ya kuridhisha katika mechi kubwa.